Bei za Majisafi na Usafi wa Mazingira zinazotolewa na zinaidhinishwa na EWURA. Kabla ya kuanza kutekeleza Bei zilizoidhinishwa, ada na malipo mengine, Mamlaka inawasilisha EWURA maombi ya kuongeza bei kutokana na Mpango Biashara wa TUWASA. Baada ya EWURA kupitia na Kujiridhisha, huandaa mkutano wa wadau wa maji ili kuwaeleza kusudio la Mamlaka la kuongeza bei. Bei mpya za huduma huanza kutumika baada ya kupitia maoni ya wadau na kutoa elimu kikamilifu kwa umma ikiwa ni pamoja na wawakilishi wa wananchi, serikali na viongozi wa dini.